Showing posts with label WORLD RABIES DAY CELEBRATIONS. Show all posts
Showing posts with label WORLD RABIES DAY CELEBRATIONS. Show all posts

Monday, September 5, 2011

WORKING TOGETHER TO MAKE RABIES HISTORY

  • Tujifunza kufanya kichaa cha mbwa kuwa Historia


Kichaa cha mbwa ni nini?
  • Kichaa cha mbwa ni ugonjwa unaosababishwa na Virusi ambavyo huwa kwenye mate ya mnyama mngonjwa.
  • Virusi hivi husambazwa kwa binadamu na wanyama kupitia kuumwa/kung’atwa na mnyama aliyeambukizwa.
  • Mara tu dalili za kichaa cha mbwa zinapoanza, matokeo yake huwa ni kifo.



Nini kinasababisha kichaa cha mbwa?

  • Kichaa cha mbwa kinasababishwa na Virusi, vimelea ambao ni wadogo kuliko bacteria.
  • Vimelea wa Kichaa cha mbwa wakiingia mwilini hushambulia na kuharibu mfumo kati wa fahamu
  • Mfumo kati wa ufahamu unajumuisha Ubongo na uti wa Mgongo.
  • Mfumo wa fahamu ulio na afya ni muhimu kwa; Kufikiri, Kuhisi, kuona, kupumua, kumeza, kula, kutembea na kuongea.

Wanyama gani wanapata kichaa cha mbwa?
Virusi vya kichaa cha mbwa vinaweza kumuingia mnyama yeyote aina ya mamalia.


  • Wanyama kama vyura, Ndege na Nyoka hawawezi kupata kichaa cha mbwa
  • Baadhi ya wanyama wanaoeneza kichaa cha mbwa ni, Mbwa, Popo, Mbweha na Paka
  • Mbwa ndiye kisababishi kikuu cha kichaa cha mbwa kwa Binadamu Duniani kote

Mnyama mwenye kichaa cha mbwa ana dalili gani?

  • Mbwa na paka wanapokuwa na kichaa cha mbwa huonyesha dalili kadhaa kama vile;
  • Kuwa na uoga na kuchanganyikiwa
Atataka kung’ata binadamu na wanyama wengine

  • “Kuogopa maji" na kushindwa kumeza kutokana na matatizo kwenye koo
  • Kudondokwa na mate kwa wingi
  • Wanyama wa mwitu wenye ugonjwa huu hubadili tabia zao kwa mfano, wanao onekana usiku peke yake huonekana wakizurura mchana.
  • Mbwa, paka, farasi, ng’ombe, kondoo na mbuzi pia huonyesha dalili za unyonge, kujiumiza au kujing’ata vile vile kutoweza kustahimili mwangaza.

Nifanye nini ili kuzuia kichaa cha mbwa?
  • Hakikisha wanyama wako wamechanjwa na afisa wa kudhibiti wanyama kuzuia kichaa cha mbwa
  • Ita wataalamu wa wanyama ukiona mnyama mgonjwa
  • Hakikisha kuwa sehemu za kutupia makombo na taka haziwavutii wanyama wa porini
  • Mnyama wa kufugwa atakiwa kuangaliwa kwa muda wa siku kumi(10) kwa dalili za kichaa cha mbwa.

Nifanye nini mnyama wangu anapomuuma mtu?


  • Mhimize mtu huyo akamwone daktari haraka iwezekanavyo.
  • Mwone daktari wako wa mifugo kubaini kama chanjo ya mnyama wako iko sawa kulingana na wakati wake.
  • Itabidi mnyama wako azuiliwe na aangaliwe kwa muda wa siku kumi (10) kwa dalili za kichaa cha mbwa.
  • Piga ripoti kwa afisa wako punde tu utakapoona dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa.
  • Baada ya uchunguzi huu, hakikisha mnyama wako amepata chanjo dhidi ya kichaa cha mbwa.


Nifanye nini mnyama wangu anapoumwa?
  • Mwone daktari wako wa mifugo ili mnyama huyo apate chanjo dhidi ya kichaa cha mbwa hata kama alikuwa keshachanjwa.
  • Itabidi umzuilie mnyama wako na kumwangalia kwa muda wa siku arobaini na tano(45) ama zaidi kwa dalili za kichaa cha mbwa.
  • Mbwa na paka ambao hawakuwa na chanjo itabidii wauwawe au wazuliwe kwa muda wamiezi sita (6).
  • Wanyama wengine isipokuwa mbwa na paka, waking’atwa, itabidii wauwawe haraka iwezekanavyo

Nifanye nini ninapoumwa na mnyama?
  • Usiwe na hofu! Safisha kidonda vizuri kwa kutumia maji mengi na sabuni
  • Mwone daktari haraka iwezekanavyo kupata chanjo dhidi ya kichaa cha mbwa na ufuate maagizo yake.
  • Wasiliana na afisa wa kudhibiti wanyama kuthibitisha kama mnyama alikuwa amechanjwa.
  • Ikiwezekana, mzuilie ama mnase mnyama wa kufugwa ili aweze kuangaliwa kwa muda wa siku kumi(10) kwa dalili za kichaa cha mbwa.
  • Ikiwa ni mnyama wa pori, jaribu kumnasa ikiwezekana. La sivyo itabidi auwawe bila kuharibu sehemu ya ubongo kwani utahitajika kuchunguzwa kama alikuwa na kichaa cha mbwa.
  • Matibabu yanayofanyika kwa wakati mwafaka baada ya kuumwa yaweza kuzuia mtu kuambukizwa na kichaa cha mbwa.


Taarifa hii imeletwa kweni na;

KENYA WOMEN VETERINARY ASSOCIATION