Monday, September 5, 2011

WORKING TOGETHER TO MAKE RABIES HISTORY

  • Tujifunza kufanya kichaa cha mbwa kuwa Historia


Kichaa cha mbwa ni nini?
  • Kichaa cha mbwa ni ugonjwa unaosababishwa na Virusi ambavyo huwa kwenye mate ya mnyama mngonjwa.
  • Virusi hivi husambazwa kwa binadamu na wanyama kupitia kuumwa/kung’atwa na mnyama aliyeambukizwa.
  • Mara tu dalili za kichaa cha mbwa zinapoanza, matokeo yake huwa ni kifo.



Nini kinasababisha kichaa cha mbwa?

  • Kichaa cha mbwa kinasababishwa na Virusi, vimelea ambao ni wadogo kuliko bacteria.
  • Vimelea wa Kichaa cha mbwa wakiingia mwilini hushambulia na kuharibu mfumo kati wa fahamu
  • Mfumo kati wa ufahamu unajumuisha Ubongo na uti wa Mgongo.
  • Mfumo wa fahamu ulio na afya ni muhimu kwa; Kufikiri, Kuhisi, kuona, kupumua, kumeza, kula, kutembea na kuongea.

Wanyama gani wanapata kichaa cha mbwa?
Virusi vya kichaa cha mbwa vinaweza kumuingia mnyama yeyote aina ya mamalia.


  • Wanyama kama vyura, Ndege na Nyoka hawawezi kupata kichaa cha mbwa
  • Baadhi ya wanyama wanaoeneza kichaa cha mbwa ni, Mbwa, Popo, Mbweha na Paka
  • Mbwa ndiye kisababishi kikuu cha kichaa cha mbwa kwa Binadamu Duniani kote

Mnyama mwenye kichaa cha mbwa ana dalili gani?

  • Mbwa na paka wanapokuwa na kichaa cha mbwa huonyesha dalili kadhaa kama vile;
  • Kuwa na uoga na kuchanganyikiwa
Atataka kung’ata binadamu na wanyama wengine

  • “Kuogopa maji" na kushindwa kumeza kutokana na matatizo kwenye koo
  • Kudondokwa na mate kwa wingi
  • Wanyama wa mwitu wenye ugonjwa huu hubadili tabia zao kwa mfano, wanao onekana usiku peke yake huonekana wakizurura mchana.
  • Mbwa, paka, farasi, ng’ombe, kondoo na mbuzi pia huonyesha dalili za unyonge, kujiumiza au kujing’ata vile vile kutoweza kustahimili mwangaza.

Nifanye nini ili kuzuia kichaa cha mbwa?
  • Hakikisha wanyama wako wamechanjwa na afisa wa kudhibiti wanyama kuzuia kichaa cha mbwa
  • Ita wataalamu wa wanyama ukiona mnyama mgonjwa
  • Hakikisha kuwa sehemu za kutupia makombo na taka haziwavutii wanyama wa porini
  • Mnyama wa kufugwa atakiwa kuangaliwa kwa muda wa siku kumi(10) kwa dalili za kichaa cha mbwa.

Nifanye nini mnyama wangu anapomuuma mtu?


  • Mhimize mtu huyo akamwone daktari haraka iwezekanavyo.
  • Mwone daktari wako wa mifugo kubaini kama chanjo ya mnyama wako iko sawa kulingana na wakati wake.
  • Itabidi mnyama wako azuiliwe na aangaliwe kwa muda wa siku kumi (10) kwa dalili za kichaa cha mbwa.
  • Piga ripoti kwa afisa wako punde tu utakapoona dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa.
  • Baada ya uchunguzi huu, hakikisha mnyama wako amepata chanjo dhidi ya kichaa cha mbwa.


Nifanye nini mnyama wangu anapoumwa?
  • Mwone daktari wako wa mifugo ili mnyama huyo apate chanjo dhidi ya kichaa cha mbwa hata kama alikuwa keshachanjwa.
  • Itabidi umzuilie mnyama wako na kumwangalia kwa muda wa siku arobaini na tano(45) ama zaidi kwa dalili za kichaa cha mbwa.
  • Mbwa na paka ambao hawakuwa na chanjo itabidii wauwawe au wazuliwe kwa muda wamiezi sita (6).
  • Wanyama wengine isipokuwa mbwa na paka, waking’atwa, itabidii wauwawe haraka iwezekanavyo

Nifanye nini ninapoumwa na mnyama?
  • Usiwe na hofu! Safisha kidonda vizuri kwa kutumia maji mengi na sabuni
  • Mwone daktari haraka iwezekanavyo kupata chanjo dhidi ya kichaa cha mbwa na ufuate maagizo yake.
  • Wasiliana na afisa wa kudhibiti wanyama kuthibitisha kama mnyama alikuwa amechanjwa.
  • Ikiwezekana, mzuilie ama mnase mnyama wa kufugwa ili aweze kuangaliwa kwa muda wa siku kumi(10) kwa dalili za kichaa cha mbwa.
  • Ikiwa ni mnyama wa pori, jaribu kumnasa ikiwezekana. La sivyo itabidi auwawe bila kuharibu sehemu ya ubongo kwani utahitajika kuchunguzwa kama alikuwa na kichaa cha mbwa.
  • Matibabu yanayofanyika kwa wakati mwafaka baada ya kuumwa yaweza kuzuia mtu kuambukizwa na kichaa cha mbwa.


Taarifa hii imeletwa kweni na;

KENYA WOMEN VETERINARY ASSOCIATION

Sunday, February 27, 2011

IMPROVING LABORATORY DIAGNOSTIC CAPABILITY OF SOMALIA PUBLIC AND PRIVATE VETERINARIANS

IMPLEMENTORS: Kenya Women Veterinary Association
VENUE: Regional Veterinary Investigation Laboratory, Garissa
17th February to 8th March, 2010


Livestock and livestock products continue to be the major source of livelihoods and food security for pastoralists and agro-pastoralists in Southern and Central Somalia. Livestock provide food (milk and meat), a source of cash (live animals and animal products), and make the major contribution to meeting household needs and family social obligations (manure, draught power, hides, skins, and dowry disbursements, etc.). However, severe and prolonged dry seasons compounded by poor infrastructure; soaring food prices and insecurity have contributed to the households resorting to harmful coping strategies such as asset stripping exemplified by the sale of productive assets such as livestock.
The Somali pastoral context is characterized by conditions that facilitate the spread of Trans-boundary Animal Diseases (TADs). This is mainly as a result of insufficient application of disease control measures which is catalyzed by the prevailing insecurity situation in the country. Other challenges that keep on resurfacing from field reports include the lack of sufficiently qualified veterinary personnel, inadequate transport infra-structure, and lack of diagnostic capacity which is a reflection of the extensive collapse of Somali infrastructure, particularly that pertaining to human and livestock disease control.
FAO Somalia awarded a consultancy to KWVA to conduct training on improving the laboratory diagnostic capability of Somali public and private veterinarians.
The objectives of this training were;
• To develop a module for training of Somali public sector and private veterinarians on basic diagnostic laboratory techniques covering components of haematology, parasitology, bacteriology and serology.

• To improve the laboratory diagnostic skills of Somali public sector and private veterinarians from Gedo and lower Juba regions through training.




Despite the fact that Somalia has not been training the veterinary professionals from the time of the civil war, the personnel were receptive to continuous veterinary education. The trainees were fully participatory and cooperative for the whole training period. They were eager to learn more about diagnostic techniques. The importance of good laboratory practice was emphasized both in theory and in practice throughout the training.
The training marks the beginning towards improving the veterinary diagnostic capacity of public and private personnel in Somalia; a region that depends solely on the livestock sector both for food security, economic growth and sustainability due to the adverse climatic conditions.
The participants were equipped with skills on basic veterinary laboratory techniques in the following areas;
• Parasitology (faecal and blood parasites)
• Bacteriology (Preparation of basic media, inoculation and preliminary identification of bacteria)
• Serology (Agglutination techniques, precipitation techniques, CFT and ELISA)

KWVA has once again proven her prowess in successfully implementing consultancies both within and outside our country.